Short story competition

Mashindano

Ili kusherehekea uzinduzi wake, Kalahari Collection imeandaa mashindano ya hadithi fupi kwa waandishi wanaoandika kwa Kifaransa, Kizungu au Kiswahili. Aina zote za hadithi fupi kama vile za uhalisia, za kihistoria, za kubuni,za barua, za kisayansi n.k zinakubalika. Washiriki hawapaswi kuwa wameshawahi kuchapisha kitabu. Katika kila lugha kati ya hizo tatu kutachaguliwa hadithi tatu bora zitakazozawadiwa, zitafsiriwe na zichapishwe na Kalahari Collection.

Jopo la majaji wa lugha ya Kiswahili

LLelo _4771957360786101514_n

Lello Mmassy

Ni Mchumi Kitaaluma, akiwa na Shahada katika Maendeleo ya Uchumi aliyohitimu kutoka Chuo Kikuu Cha Mwalimu Nyerere kinachopatikana Dar es Salaam, Tanzania. Kikazi, Lello ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Wateja katika kampuni ya Utengenezaji wa Vinywaji ya Tanzania Breweries Limited (TBL). Lello ameandika vitabu kadhaa mashuhuri ambavyo baadhi vimeshinda tuzo ya ubora wa Fasihi ya Mabati-Cornell Kiswahili Prize for African Literature kwa kitabu chake cha Mimi na Rais. Vilevile, Lello Mmassy ni Mwanzilishi wa Programu tumishi iitwayo Simulizi Africa inayopatikana katika duka la programu la Google, ‘Playstore’ na pia ni mwanzilishi mwenza wa kampuni ya Serengeti Bytes inayojishughulisha na Mahusiano kwa Umma, Masoko, Uchapishaji, na Vyombo vya Habari. Lello ni mpenzi na mfuatiliaji mkubwa wa masuala ya Fasihi ya ndani na nje ya Afrika.

Nema 88_n

Neema George Mturo

Dkt Neema George Mturo ni Mhadhiri mzoefu wa somo la Fasihi ya Kiswahili na Isimu kwa upande wa Semantiki na Pragmatiki ya Kiswahili katika Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira, Tanzania. Ana shahada ya Uzamivu katika Fasihi ya Kiswahili kutoka katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, shahada ya Umahiri wa Fasihi ya Kiswahili kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam na shahada ya Kwanza katika Sayansi ya Siasa na Lugha kutoka nayo katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam nchini Tanzania. Aidha Dkt Neema Mturo pia ni mwandishi mbobevu wa vitabu vya Riwaya, Tamthiliya, Ushairi Hadithi Fupi na Semantiki & Pragmatiki ya Kiswahili, Vilevile ni mwandishi wa makala mbalimbali za fasihi ya Kiswahili katika majarida .

Mutani-Elias

Elias Mutani

Ni mwandishi wa riwaya na vitabu vingine, ni mhariri, mfasiri na mchapishaji kutoka Bagamoyo, Tanzania. Ni mshiriki katika timu ya ufasiri ya Commonwealth Foundation na Caine Prize Kutoka Uingereza. Alikuwa jaji katika shindano la ‘Andika na Soma’ linaloshirikisha waandishi chipukizi msimu wa 2016 na 2017, pia mkufunzi wa waandishi wa Kiafrika kutoka Mradi wa Afroyoungadult chini ya Goethe Institut. Mwaka 2016 na 2017 vitabu vyake ‘HUMAN POACHERS’ na ‘THE GOLDEN PAPERKNIFE’ vilishinda Tuzo ya Burt ya Uandishi wa Fasihi ya Kiafrika nchini Tanzania. Kando ya uandishi; Elias ni mnasihi anayehudumia vituo mbalimbali vya watoto na yatima Afrika Mashariki.